Kabla ya Mapinduzi ya 1964
Afisi ya Mwanasheria Mkuu ni miongoni mwa taasisi kongwe zilizoanzishwa Zanzibar katika kipindi cha utawala wa kikoloni mnamo mwaka 1913–1914. Kazi yake kuu ilikuwa kutoa ushauri wa kisheria kwa Serikali na kusimamia masuala ya kisheria kwa niaba ya Serikali.
Mwaka 1926 Mwanasheria Mkuu alikuwa miongoni mwa wajumbe wa Baraza la Kutunga Sheria na Utawala, akiendelea kushiriki katika masuala ya kisheria hadi kipindi cha Mapinduzi ya mwaka 1964.