Masharti ya Matumizi
Kwa kutumia tovuti hii, mtumiaji anakubali kuzingatia masharti na taratibu za matumizi ya taarifa na huduma zinazotolewa na Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar.
Matumizi Sahihi
Mtumiaji anatakiwa kutumia tovuti hii kwa madhumuni halali na kwa kuzingatia sheria, kanuni na maadili ya matumizi ya huduma za mtandao.
Usahihi wa Taarifa
Afisi inajitahidi kuhakikisha taarifa zilizowekwa kwenye tovuti ni sahihi na za wakati. Hata hivyo, taarifa zinaweza kubadilika kulingana na mazingira au marekebisho ya kiutawala na kisheria.
Hakimiliki
Maudhui yote yaliyopo kwenye tovuti hii ni mali ya Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar isipokuwa pale ilipoelezwa vinginevyo.